Swali: Mwenye kumwambia baba yake ´ewe kafiri` ukafiri unamrudilia yeye mwenyewe…
Jibu: Hili halimuhusu baba yake tu. Akimwambia muislamu yeyote ´ewe kafiri` ilihali sio kafiri, maneno yake yanamrulia yeye mwenyewe – tunaomba kinga kwa Allaah. Vivyo hivyo akimwambia ´ewe khabithi`, ´Allaah akulaani` au mfano wa maneno kama hayo, ikiwa hastahiki hilo, maneno haya hayaendi patupu. Bali madhambi na khatari yake inamrudilia yeye mwenyewe, ni mamoja ikiwa atamwambia baba yake au mtu mwingine. Lakini hata hivyo akimwambia baba yake hivo ni khatari zaidi kwa sababu huku ni kuasi haki za wazazi. Allaah (Jalla wa ´Alaa) amesema:
وَلَا تَنْهَرْهُمَا وَقُل لَّهُمَا قَوْلًا كَرِيمًا
“Na wala usiwakemee; na waambie maneno ya heshima.” (17:23)
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Kitaab Ahaadiyth-il-Fitnah (2) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/ftn–1432-08-16.mp3
- Imechapishwa: 21/04/2015
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)
Related
Wanazuoni ndio wana haki ya kukufurisha na kufanya Tabdiy´
Swali: Muislamu anayo haki ya kumkufurisha au kumfanyia Tabdiy´ kila ambaye atatumbukia katika kufuru au Bid´ah? Jibu: Kuwa na haraka ya kuwahukumu watu na kuwakufurisha na kuwafanyia Tabdiy´, hili halijuzu isipokuwa kwa wanazuoni ambao wanajua mipaka ya kufuru, Bid´ah, kuritadi na sababu zake wanazijua wanazuoni. Hili ni jambo khaswa kwa…
In "Vidhibiti vya Takfiyr na kanuni zake"
Mtoto muislamu kuwahudumia wazazi makafiri
Swali: Je, ni lazima kwa mtoto kuwahudumia wazazi kwa hali zote au ni pale tu ambapo wanakuwa ni mafakiri? Jibu: Wajibu wake ni yeye kutomuhitaji yeyote na kujitosheleza mwenyewe. Swali: Je, ni wajibu kwa mtoto muislamu kumpa matumizi baba yake kafiri? Jibu: Ndio, ni katika kumfanyia wema mzazi hata kama…
In "Kuwatendea wema wazazi"
Baba yake anamkatalia kuhiji
Swali: Mimi ni kijana ambaye nina uwezo wa kuhiji na bado sijahiji ile hajj ya kwanza. Baba yangu ananikatalia kuhiji. Ni ipi hukumu ya kukaa kwangu na hukumu ya baba yangu kunikatalia hajj? Jibu: Ni lazima kwake kuhiji hata kama baba yake atamkatalia. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema: "Hakika si…
In "Kuwatendea wema wazazi"