Swali: Kuna wanaosema kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anatoka katika umbile la uanaadamu pindi anapoteremshiwa Wahy. Je, maneno haya ni sahihi?
Jibu: Ni maneno batili. Haijuzu kusema juu ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) jambo ambalo ndani yake lina kashfa. Anatoka katika umbile la uanaadamu! Anakuwa vipi sahihi? Je, anakuwa mwendawazimu? Anakuwa katika hali ipi? Kwa maana akitoka katika umbile la uanaadamu atakuwa vipi? Ni mwanaadamu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wala hatoki katika umbile la uanaadamu. Kusema kwamba Wahy unamtia uzito hili ni sahihi. Pale anapoteremkiwa na Wahy unamtia uzito:
إِنَّا سَنُلْقِي عَلَيْكَ قَوْلًا ثَقِيلًا
”Hakika Sisi tutaweka juu yako kauli nzito.” (73:05)
Ni kweli kuwa upokeaji wa Wahy unamtia uzito. Ama kuhusu kwamba anatoka katika umbile la uanaadamu, haya ni maneno batili. Ni kumtukana Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Kitaab Ahaadiyth-il-Fitnah (2) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/ftn–1432-08-16.mp3
- Imechapishwa: 21/04/2015
Swali: Kuna wanaosema kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anatoka katika umbile la uanaadamu pindi anapoteremshiwa Wahy. Je, maneno haya ni sahihi?
Jibu: Ni maneno batili. Haijuzu kusema juu ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) jambo ambalo ndani yake lina kashfa. Anatoka katika umbile la uanaadamu! Anakuwa vipi sahihi? Je, anakuwa mwendawazimu? Anakuwa katika hali ipi? Kwa maana akitoka katika umbile la uanaadamu atakuwa vipi? Ni mwanaadamu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wala hatoki katika umbile la uanaadamu. Kusema kwamba Wahy unamtia uzito hili ni sahihi. Pale anapoteremkiwa na Wahy unamtia uzito:
إِنَّا سَنُلْقِي عَلَيْكَ قَوْلًا ثَقِيلًا
”Hakika Sisi tutaweka juu yako kauli nzito.” (73:05)
Ni kweli kuwa upokeaji wa Wahy unamtia uzito. Ama kuhusu kwamba anatoka katika umbile la uanaadamu, haya ni maneno batili. Ni kumtukana Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Kitaab Ahaadiyth-il-Fitnah (2) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/ftn–1432-08-16.mp3
Imechapishwa: 21/04/2015
https://firqatunnajia.com/hali-ya-mtume-anapoteremshiwa-wahy/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)