Faqiyh Abu ´Aliy bin al-Bannaa´ amesema:
“al-Hallaaj alikuwa akidai kuwa ni mungu na akisema kuwa uungu umekita ndani ya mwanadamu. Pindi waziri ´Aliy bin ´Iysaa alipomleta akamuona kuwa mtu huyo hamairi vizuri si Qur-aan, Fiqh wala Hadiyth. Bora kwako ni wewe kujifunza mambo ya faradhi na ya twahara kuliko kuandika mambo ambayo hutambui chochote juu yake. Ole wako! Ni mara ngapi unawaandikia watu: “Ametukuka ambaye ana mwanga wa kung´ara!” Hakika una haja kubwa ya adabu.” Baada ya hapo akaamrisha asubulubiwe, mara ya kwanza alisulubiwa upande wa mashariki na kisha baadaye akasulubiwa upande wa magharibi. Ilipatikana katika vitabu vyake ameandika:
“Mimi ndiye niliwazamisha watu wa Nuuh, mimi ndiye nimewaangamiza kina ´Aad na Thamuud.”
Alikuwa akiwaambia wafuasi wake:
“Wewe ndiye Nuuh, wewe ndiye Muusa na wewe ndiye Muhammad.”
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (14/327)
- Imechapishwa: 16/11/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)