Swali: Je, tuna haki ya kumwacha mnaswara kwa lengo la kuongozwa na Allaah akasoma Qur-aan iliyotarjumiwa hata kama atakuwa hana wudhuu´?
Jibu: Kulingania katika njia ya Allaah ndio mfumo wa Mitume. Amesema (Ta´ala):
قُلْ هَـٰذِهِ سَبِيلِي أَدْعُو إِلَى اللَّـهِ ۚ عَلَىٰ بَصِيرَةٍ أَنَا وَمَنِ اتَّبَعَنِي ۖ وَسُبْحَانَ اللَّـهِ وَمَا أَنَا مِنَ الْمُشْرِكِينَ
“Sema: “Hii ndio njia yangu nalingania kwa Allaah, juu ya ujuzi mimi na anayenifuata. Na Utakasifu ni wa Allaah, nami si miongoni mwa washirikina”.” (12:108)
Kumpa nuskha iliyo na tarjama ya maana ya Qur-aan tukufu ni miongoni mwa aina za kulingania katika dini ya Allaah. Ni sawa kufanya hivo.
- Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (4/41)
- Imechapishwa: 22/08/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)