Imaam Ibn Qudaamah (Rahimahu Allaah) amesema:
Njia ni haki. Wema watavuka na waasi watatumbukia humo.
MAELEZO
Njia maana yake kilugha ni njia hivohivo. Njia maana yake katika Shari´ah ni daraja itayowekwa juu ya Moto ili watu wapite juu yake kuelekea Peponi. Ni kitu kimethibiti kwa Qur-aan, Sunnah na maneno ya Salaf. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَإِن مِّنكُمْ إِلَّا وَارِدُهَا
“Na hakuna yeyote miongoni mwenu isipokuwa ataufikia.”[1]
´Abdullaah bin Mas´uud, Qataadah na Zayd bin Aslam wamefasiri kuwa ni kupita juu ya Njia. Kuna kikosi katika wao, akiwemo Ibn ´Abbaas, ambao wamefasiri kwamba ni kuingia ndani ya Moto lakini baadaye wataokolewa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kisha itawekwa daraja juu ya Moto na utashuka uombezi na watasema: “Ee Allaah! Tusalimishe! Tusalimishe!”[2]
Kuna maafikiano juu yake.
Ahl-us-Sunnah wameafikiana juu ya kuthibiti kwake.
[1] 19:71
[2] al-Bukhaariy (7439) na Muslim (183, 302).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 125-126
- Imechapishwa: 04/12/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)