Imani inazidi kwa utiifu na inashuka kwa maasi. Amesema (Ta´ala):
فَزَادَهُمْ إِيمَانًا
“Yakawazidishia imani.”[1]
لِيَزْدَادُوا إِيمَانًا مَّعَ إِيمَانِهِمْ
”Ili awazidishie imani pamoja na imani zao.”[2]
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atatolewa ndani ya Moto yule aliyesema “hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah” na moyoni mwake mna imani kiasi cha punje ya ngano, mbegu ya haradali au vumbi nafaka.”[3]
al-Bukhaariy amepokea mfano wake.
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akafanya imani ni yenye kutofautiana. Kukithibiti kuzidi kwake ndio kumethibiti kushuka kwake. Kwa sababu chenye kuzidi ni lazima kabla ya hapo kiwe kimeshuka ndio kikazidi.
[1] 03:173
[2] 48:04
[3] al-Bukhaariy (44) na Muslim (193).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 99
- Imechapishwa: 07/11/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)