Allaah (Ta´ala) ameamrisha kushikamana na Qur-aan na akasema:
وَاعْتَصِمُوا بِحَبْلِ اللَّـهِ جَمِيعًا وَلَا تَفَرَّقُوا
”Na shikamaneni kwa kamba ya Allaah nyote pamoja wala msifarikiane.”
Kamba ya Allaah (Ta´ala) ni Kitabu Chake. Zayd bin Arqam amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Zindukeni! Hakika mimi nimekuachieni vizito viwili ambapo kimoja wapo ni Kitabu cha Allaah, nayo ndio kamba ya Allaah. Yule mwenye kukifuata ameongoka, na yule mwenye kukiacha amepotea.”[1]
Ibn Mas´uud (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Hakika njia hii ni yenye kuhudhuriwa na mashaytwaan waitao: “Ee mja wa Allaah, hii hapa njia!” Shikamaneni na njia ya Allaah. Kwani hakika njia ya Allaah ni Qur-aan.”[2]
Ibn Mas´uud (Radhiya Allaahu ´anh) amesema tena:
“Hakika Qur-aan hii ni ndio kamba ya Allaah, nuru, shifaa yenye kunufaisha, kinga kwa yule mwenye kushikamana nayo na uokozi kwa yule mwenye kuifuata.”[3]
al-Kirmaaniy amesema kuhusiana na maneno Yake Allaah (Ta´ala):
وَاعْتَصِمُوا بِحَبْلِ اللَّـهِ جَمِيعًا وَلَا تَفَرَّقُوا
”Na shikamaneni kwa kamba ya Allaah nyote pamoja wala msifarikiane.”[4]
“Makusudio ya kamba ni Qur-aan na Sunnah… kwa sababu vyote viwili vinapelekea katika malengo, nazo ni thawabu, kama ambavo kamba inapelekea katika maji ndani ya kisima na mengineyo.”[5]
´Allaamah ´Aliyal-Qaariy amemkosea juu ya hilo na akasema:
“Kilichotangaa ni kwamba kamba inakusudiwa Qur-aan, kama ilivyopokelewa katika baadhi ya Hadiyth. Hata hivyo kushikamana na Qur-aan kunapelekea vilevile kushikamana na Sunnah kwa sababu Allaah (Ta´ala) amesema:
وَمَا آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانتَهُوا
”Kile alichokupeni Mtume basi kichukueni na kile alichokukatazeni basi kiacheni.”[6][7]
[1] Muslim (2408).
[2] ad-Daarimiy katika ”as-Sunan”.
[3] ad-Daarimiy katika ”as-Sunan”.
[4] 3:103
[5] al-Kawaakib ad-DaraariyfiySharhSwahiyh al-Bukhaariy (25/28).
[6] 59:7
[7]Mirqaat-ul-Mafaatiyh (1/365).
- Muhusika: Shaykh ´Abdus-Salaam bin Barjas Aal ´Abdil-Kariym
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Hujaj al-Qawiyyah ´alaa anna Wasaa-il-ad-Da´wah Tawqiyfiyyah, uk. 21-22
- Imechapishwa: 08/05/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)