Kushuka kwa Mola kila usiku katika mbingu ya chini ni jambo ambalo limesihi kupokelewa kwa maafikiano. al-Bukhaariy na Muslim wameipokea kupitia kwa Maalik bin Anas, kutoka kwa az-Zuhriy, kutoka kwa al-Agharr na Abu Salamah, kutoka kwa Abu Hurayrah.
Abu ´Aliy Zaahir bin Ahmad ametukhabarisha: Abu Ishaaq Ibraahiym bin ´Abdis-Swamad ametuhadithia: Abu Musw´ab ametuhadithia: Maalik ametuhadithia …:
Abu Bakr bin Zakariyyaa ametuhadithia: Abu Haatim Makkiy bin ´Abdaan ametuhadithia: Muhammad bin Yahyaa ametuhadithia: Nilimsomea Ibn Naafiy´ na Mutwarrif amenihadithia, kutoka kwa Maalik…
Abu Bakr bin Zakariyyaa ametuhadithia: Abul-Qaasim ´Ubaydullaah bin Ibraahiym bin Baakuuyah amenikhabarisha: Yahyaa bin Muhammad ametuhadithia: Yahyaa bin Yahyaa ametuhadithia: Nilimsomea Maalik, kutoka kwa Ibn Shihaab az-Zuhriy, kutoka kwa Abu ´Abdillaah al-Agharr na Abu Salamah, kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) aliyesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mola wetu (Tabaarak wa Ta´ala) hushuka kila usiku katika mbingu ya chini ya dunia pale kunapobaki theluthi ya mwisho ya usiku na anasema: “Nani anayeniomba Nimpe? Ni nani anayeniuliza Nimpe? Ni nani anayetaka nimsamehe Nimghufurie?”
Hadiyth hii imepokelewa kupitia njia nyingi kutoka kwa Abu Hurayrah.
al-Awzaa´iy ameipokea kutoka kwa Yahyaa bin Abiy Kathiyr, ambaye amepokea kutoka kwa Abu Salamah, ambaye amepokea kutoka kwa Abu Hurayrah.
Yaziyd bin Haaruun na maimamu wengine wameipokea kutoka kwa Muhammad bin ´Amr, ambaye ameipokea kutoka kwa Abu Salamah, ambaye ameipokea kutoka kwa Abu Hurayrah.
Maalik ameipokea kutoka kwa az-Zuhriy, ambaye ameipokea kutoka kwa al-A´raj, ambaye ameipokea kutoka kwa Abu Hurayrah.
Maalik ameipokea kutoka kwa az-Zuhriy, ambaye ameipokea kutoka kwa Sa´iyd bin al-Musayyab, ambaye ameipokea kutoka kwa Abu Hurayrah.
´Ubaydullaah bin ´Amr ameipokea kutoka kwa Sa´iyd bin Abiy Sa´iyd al-Maqburiy, ambaye ameipokea kutoka kwa Abu Hurayrah.
´Abdul-A´laa bin Abiyl-Musaawir na Bashiyr bin Sulaymaan wameipokea kutoka kwa Abu Haazim, ameipokea kutoka kwa Abu Hurayrah.
- Muhusika: Imaam Abu ´Uthmaan Ismaa´iyl bin ´Abdir-Rahmaan as-Swaabuuniy (afk. 449)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ´Aqiydat-us-Salaf wa Aswhaab-il-Hadiyth, uk. 198-206
- Imechapishwa: 06/12/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)