Katika Aayah moja Amesema:
يَوْمَ يَجْمَعُ اللَّـهُ الرُّسُلَ فَيَقُولُ مَاذَا أُجِبْتُمْ ۖ قَالُوا لَا عِلْمَ لَنَا ۖ إِنَّكَ أَنتَ عَلَّامُ الْغُيُوبِ
“Siku Allaah atawakusanya Mitume na kuwaambia: “Mlijibiwa nini?” Watasema: “Hatuna ujuzi nalo, kwani hakika Wewe unayajua mno yenye kufichikana.”[1]
Katika Aayah nyingine Amesema:
وَيَقُولُ الْأَشْهَادُ هَـٰؤُلَاءِ الَّذِينَ كَذَبُوا عَلَىٰ رَبِّهِمْ
”… mashahidi watasema ”hawa ndio wale waliomzulia uwongo Mola wao!””[2]
Wanauliza kwamba ni vipi wanasema ”hawajui”, kisha kwamba ”hawa ndio waliomsemea uwongo Mola wao”. Wakadai kuwa Qur-aan ni yenye kujigonga.
Kuhusu maneno Yake:
يَوْمَ يَجْمَعُ اللَّـهُ الرُّسُلَ فَيَقُولُ مَاذَا أُجِبْتُمْ ۖ قَالُوا لَا عِلْمَ لَنَا ۖ إِنَّكَ أَنتَ عَلَّامُ الْغُيُوبِ
“Siku Allaah atawakusanya Mitume na kuwaambia: “Mlijibiwa nini?” Watasema: “Hatuna ujuzi nalo, kwani hakika Wewe unayajua mno yenye kufichikana.”
atawauliza pale Moto utapopumua. Atawauliza walijibu vipi juu ya upwekeshaji, akili yao ipotee wakati Moto utakapotoa pumzi na waseme:
لَا عِلْمَ لَنَا
“Hatuna ujuzi nalo… ”
Kisha baadaye fahamu yao irudi na waseme:
هَـٰؤُلَاءِ الَّذِينَ كَذَبُوا عَلَىٰ رَبِّهِمْ
”… hawa ndio wale waliomzulia uwongo Mola wao”
Hii ndio tafsiri ya yale waliyoyatilia mashaka mazanadiki[3].
[1] 5:109
[2] 11:18
[3] Ibn ´Aqiyl al-Hanbaliy amesema:
”Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) ameandika kitabu kinachoitwa ”ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah waz-Zanaadiqah wal-Qadariyyah.” (al-Aadaab ash-Shar´iyyah (1/274))
Ibn Taymiyyah amesema:
”Kama alivosema Imaam Ahmad katika kitabu chake ”ar-Radd ´alaaz-Zanaadiqah wal-Jahmiyyah.” (Tafsiyr Suurat-il-Ikhlaasw, uk. 239)
Ibn Kathiyr amesema:
”… na hivo ndivo alivosema Ahmad bin Hanbal katika kitabu ”ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah” (Tafsiyr al-Qur-aan al-´Adhwiym (3/304))
Ibn Hajar al-´Asqalaaniy amesema:
”Amesema waziwazi Ahmad katika kitabu “ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah.” (Fath-ul-Baariy (13/598))
- Muhusika: Imaam Ahmad bin Hanbal (afk. 241)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah waz-Zanaadiqah, uk. 74-76
- Imechapishwa: 14/04/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)