Swali: Imekuja katika Hadiyth ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliona Swafiyyah amechukulia vibaya ambapo Swafiyyah (Radhiya Allaahu ´anhaa) akamwambia ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa):
“Je, unaonaje umridhishe Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na nikupe siku yangu… ?”
Kuna jambo lenye kutatiza katika Hadiyth: je, zawadi inakubaliwa katika uombezi?
Jibu: Hapana, isipokuwa akiliruhusu hilo mume. Mume alikiruhusu hilo haina neno.
Swali: ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) alikubali siku ya Swafiyyah (Radhiya Allaahu ´anhaa)?
Jibu: Ni siku ya Sawdah. Sawdah alipotaka kuachwa akamwambia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuwa anamgawia siku yake ´Aaishah ambapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akalikubali hilo. Kwa hivyo ni sawa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akikubali kutoka kwa mke wake.
Swali: Haizingatiwi kuwa ni katika kukubali zawadi katika uombezi?
Jibu: Hapana, haina neno. Kwa sababu huku ni kudondosha haki yake.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23096/ما-حكم-الهدية-التي-تعطى-في-الشفاعة
- Imechapishwa: 01/11/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)