Swali: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwakataza Maswahabah waliposema:
”Wewe ni bwana wetu.”
ambapo akasema kuwa Bwana ni Allaah. Vipi tutaoanisha hilo na maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliposema:
”Mimi ni bwana wa wana wa Aadam na si fakhari”?
Jibu: Aliwaambia hivo ili kusiwapelekei katika kuchupa mpaka. Alichelea juu yao kuchupa mpaka. Aliwaambia:
”Semeni maneno yenu au baadhi ya maneno yenu na wala asikufitinisheni shaytwaan. Kuhusu baada ya kufa kwake hakuna tena…
Jibu: Je, hakuwa akieleza kuwa yeye ni bwana wa wana wa Aadam?
Jibu: Yeye ni kiongozi wa wana wa Aadam. Lakini hakupenda kusifiwa hivo katika uhai wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Alichelea juu yao kupetuka mpaka.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22244/الجمع-بين-حديثي-سيد-ولد-ادم-والسيد-الله
- Imechapishwa: 19/01/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)