Swali: Je, bora kwangu ni kusoma Qur-aan au kuswali swalah inayopendeza ninapofika msikitini kabla ya kuadhiniwa?
Jibu: Aswali Raatibah. Kwa mfano Dhuhr kuna Rak´ah nne kabla yake na baina ya kila adhaana na iqaamah kuna swalah. Kukiadhiniwa basi inapendeza kwa walioko msikitini kuswali Rak´ah mbili.
Swali: Wakati mwingine kama mfano wa baada ya Maghrib hakuna Raatibah.
Jibu: Haijalishi kitu aswali Rak´ah mbili. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Baina ya kila adhaana mbili kuna swalah. Baina ya kila adhaana mbili kuna swalah.”
Amesema tena:
“Swalini kabla ya Maghrib. Swalini kabla ya Maghrib.”
Kisha akasema:
“Kwa anayetaka.”
Zote hizi ni swalah zinazopendeza baina ya adhaana mbili; Maghrib, ´Ishaa na ´Aswr pia. Kuhusu Dhuhr kuna Raatibah kabla yake. ´Aswr inapendeza kabla yake kuswali Rak´ah nne. Fajr kuna Raatibah kabla yake baina ya adhaana na iqaamah.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23031/ماذا-يسن-لمن-حضر-قبل-الاذان-وبعده
- Imechapishwa: 20/10/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)