Swali: Vipi kuhusu kudumu kunyanyua mikono wakati wa kuomba du´aa baada ya swalah ya faradhi?
Jibu: Si jambo limewekwa katika Shari´ah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwa akinyanyua mikono yake baada ya swalah ya faradhi.
Swali: Kwa hivyo inazingatiwa ni Bid´ah?
Jibu: Haitakikani. Azinduliwe mtu huyo.
Swali: Nikimuona anayefanya hivo?
Jibu: Kama ananyanyua baada ya swalah ya faradhi azinduliwe. Ni jambo lisilofaa. Ni jambo halikuwekwa katika Shari´ah. Bali ni Bid´ah. Akifanya baadhi ya nyakati katika swalah inayopendeza, Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alifanya hivo katika swalah inayopendeza.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23030/حكم-مداومة-رفع-اليدين-والدعاء-بعد-الفريضة
- Imechapishwa: 20/10/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)