Swali: Je, ni kweli kwamba mtu kudumu akiswali shufwa kunapelekea Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumuombea anayefanya hivo?
Jibu: Sijui chochote kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) juu ya hilo. Muumini anaswali shufwa mchana na usiku. Hii ndio Sunnah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Swalah ya usiku na mchana ni [Rak´ah] mbilimbili.”
Witr inakuwa usiku ambayo mtu anamalizia swalah yake kwa Rak´ah moja. Vilevile katika baadhi ya aina ya swalah ya khofu mtu anaswali Rak´ah moja.
Sunnah swalah siku zote inakuwa shufwa isipokuwa Maghrib ambayo ni Witr. Allaah ameifaradhisha Witr kwa Rak´ah tatu. Kuhusu Dhuhr, ´Aswr, ´Ishaa na Fajr zote ni shufwa. Vivyo hivyo swalah zote za kujitolea zinaswaliwa shufwa; Rak´ah mbilimbili. Isipokuwa Witr ndio huswaliwa Rak´ah moja. Kadhalika katika baadhi ya aina ya swalah ya khofu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliswali Rak´ah moja wakati alipokutana na maadui.
Kuhusu Hadiyth kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliswali shufwa sijui kuwa ina msingi.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/15802/هل-المدوامة-على-صلاة-الشفع-تودي-الى-شفاعة-النبي-ﷺ
- Imechapishwa: 08/04/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)