Alikuwa ni msichana wa nne kutoka katika nyumba ya kinabii.
Inasemekana kwamba aliolewa na ´Utaybah bin Abiy Lahab kisha baadaye akamwacha.
Aliingia katika Uislamu na akahajiri baada ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Wakati dada yake Ruqayyah alipofariki, akamuoza (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa ´Uthmaan. Alikuwa bado ni bikira. Alimuoa katika Rabiy´ al-Awwal mwaka wa 03. Hata hiyo hakumzalia watoto.
Alifariki katika Sha´baan mwaka wa 09. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Lau ningelikuwa na wasichana kumi, basi ningeliwaoza kwa ´Uthmaan.”[1]
Anas bin Maalik ameeleza kwamba alimuona Umm Kulthum bint Rasuulillaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimuona akiwa na shuka ya juu ya iliochanganywa na hariri[2].
Anas bin Maalik amesema:
”Nilimuona Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akikaa karibu na kaburi lake na macho yake yanatokwa na machozi. Akasema: ”Katika yenu kuna yeyote ambaye hakufanya jimaa usiku?” Abu Twalhah akasema: ”Mimi.” Ndipo akasema: ”Shuka chini.” Ndipo akashuka chini kwenye kaburi.”[3]
[1] at-Twabaqaat al-Kubraa (8/38).
[2] al-Bukhaariy (10/252).
[3] al-Bukhaariy (3/126).
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn adh-Dhahabiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (2/252-253)
- Imechapishwa: 05/10/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)