Tunaamini pia kuwa Allaah ni Mwenye kusikia na Mwenye kuona. Anasikia kila tunachokisema hata kama kitakuwa kidogo. Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) amesema:
أَمْ يَحْسَبُونَ أَنَّا لَا نَسْمَعُ سِرَّهُمْ وَنَجْوَاهُم ۚ بَلَىٰ وَرُسُلُنَا لَدَيْهِمْ يَكْتُبُونَ
“Au wanadhania kwamba Sisi hatusikii siri zao na minong’ono yao? Sivyo! [tunasikia]na wajumbe wetu wako kwao wanaandika.” (43:80)
يَعْلَمُ السِّرَّ وَأَخْفَى
“.. Yeye anajua ya siri na yanayofichika zaidi.” (20:07)
bi maana kilichofichikana zaidi kuliko siri. Hichi ni kile ambacho mtu anajiambiza ndani ya nafsi yake. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَلَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ وَنَعْلَمُ مَا تُوَسْوِسُ بِهِ نَفْسُهُ
“Hakika Tumemuumba mtu na tunajua yale [yote] yanayomshawishi nafsi yake.” (10:16
Kilichomo ndani ya nafsi Allaah anakijua hata kama hakijajidhihirisha kwa mja.
Vilevile Allaah (´Azza wa Jall) ni Mwenye kuona. Anamuona mdudu mchungu mweusi, kwenye mwamba mweusi na kwenye usiku wenye giza. Mdudu mchungu huyo hafichikani kwake.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Riyaadh-is-Swaalihiyn (01/436-437)
- Imechapishwa: 12/06/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)