Swali: Mtu akate swawm kwa maji na tende au chochote kingine?
Jibu: Kwa chochote kitachomuwepesikia. Lakini bora ni kwa tende. Tende tosa ndio bora zaidi, kisha tende za kawaida halafu maji. Hapana vibaya pia akikata swawm kwa mkate au kitu kingine.
Swali: Akikata swawm kwa kitu kingine?
Jibu: Hapana vibaya. Lakini bora ni kwa tende tosa au tende za kawaida. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Afutari kwa tende, kwani zina baraka. Asipopata, basi afutari kwa maji, kwani ni yenye kutwahirisha.”
Anas (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akifutari kwa tende tosa, asipopata akifutari kwa tende, asipopata anafutari kwa glasi ya maji.”
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22805/حكم-الافطار-على-غير-التمر-او-الماء
- Imechapishwa: 24/03/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)