Swali: Je, inafaa kufunga siku sita za Shawwaal ilihali nadaiwa swawm ya mwezi wa Ramadhaan? Nina shauku kubwa ya kufanya hivo lakini siwezi kulipa kutokana na mambo fulani ikiwa ni pamoja na masomo, maisha ya kindoa na mengineyo. Naomba maelekezo na Allaah akujaze kheri.
Jibu: Kilicho cha lazima ni kulipa deni kwanza kabla ya kuanza kufunga siku sita. Mtu asifunge siku sita za Shawwaal isipokuwa baada ya kulipa deni la Ramadhaan. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule atakayefunga Ramadhaan kisha akaifuatishia [siku] sita za Shawwaal, basi anakuwa kama amefunga mwaka mzima.”[1]
Ambaye anadaiwa Ramadhaan hajafunga na akaimaliza Ramadhaan. Amebakiza siku. Siku sita hizi zinaifuatia Ramadhaan. Kwa hivyo ni lazima kwa mtu kulipa deni kwanza ndio afunge siku sita.
[1] Muslim (1164).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/9766/حكم-صيام-الست-من-شوال-لمن-كان-عليه-قضاء
- Imechapishwa: 05/05/2022
Swali: Je, inafaa kufunga siku sita za Shawwaal ilihali nadaiwa swawm ya mwezi wa Ramadhaan? Nina shauku kubwa ya kufanya hivo lakini siwezi kulipa kutokana na mambo fulani ikiwa ni pamoja na masomo, maisha ya kindoa na mengineyo. Naomba maelekezo na Allaah akujaze kheri.
Jibu: Kilicho cha lazima ni kulipa deni kwanza kabla ya kuanza kufunga siku sita. Mtu asifunge siku sita za Shawwaal isipokuwa baada ya kulipa deni la Ramadhaan. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule atakayefunga Ramadhaan kisha akaifuatishia [siku] sita za Shawwaal, basi anakuwa kama amefunga mwaka mzima.”[1]
Ambaye anadaiwa Ramadhaan hajafunga na akaimaliza Ramadhaan. Amebakiza siku. Siku sita hizi zinaifuatia Ramadhaan. Kwa hivyo ni lazima kwa mtu kulipa deni kwanza ndio afunge siku sita.
[1] Muslim (1164).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/9766/حكم-صيام-الست-من-شوال-لمن-كان-عليه-قضاء
Imechapishwa: 05/05/2022
https://firqatunnajia.com/siku-sita-za-shawwaal-kwa-anayedaiwa-ramadhaan/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)