Mwenye janaba kutawadha kisha akaketi msikitini

Swali: Vipi ikiwa mtu yuko na janaba akatawadha na kukaa msikitini?

Jibu: Maoni sahihi ni kwamba asiketi mpaka kwanza akoge. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

“Mimi siuhalalishi msikiti kwa mwenye hedhi na mwenye janaba.”

Imepokelewa kwamba wako baadhi ya Maswahabah walikuwa wakiketi hali ya kuwa na janaba. Pengine hawakufikiwa na Hadiyth hiyo. Allaah (Subhaanah) amesema:

وَلَا جُنُبًا إِلَّا عَابِرِي سَبِيلٍ غَفُورًا

”.. na wala mkiwa mna janaba isipokuwa mmo safarini… ”[1]

Bi maana hali ya kuwa anapita tu msikitini.

[1] 04:43

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22816/حكم-جلوس-الجنب-في-المسجد
  • Imechapishwa: 26/08/2023