Swali: Ni kipi kinachopewa kipaumbele katika Shari´ah; kilicho na usalama au chepesi?
Jibu: Kilicho na usalama inapokuhusiana na utatizi.
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katu hakuwa na uwezo wa kufanya mambo mawili isipokuwa anafanya lile ambalo ni lepesi zaidi. Hili linahusiana na pale ambapo yote mawili yamo katika Shari´ah. Katika hali hii mtu anafuata lile ambalo ni lepesi. Mfano wa hili ni swalah katika safari. Inajuzu kuswali Rakaa kamilifu, na ndio asli, lakini hata hivyo kufupisha [swalah] ndio bora zaidi kwa sababu ni Sunnah ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika safari. Katika hali hii ni bora zaidi kuchukua njia sahali kuliko kutendea kazi asli.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (34) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/ighastah%20-%201%20-%202%20-%201436.mp3
- Imechapishwa: 17/06/2015
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)