Swali: Je, inafaa kwa mtu anayeswali swalah inayopendeza kunyanyua sauti yake ndani yake?
Jibu: Ndio, katika swalah ya usiku.
Swali: Mchana?
Jibu: Hapana, Sunnah ni kusoma kimyakimya. Swalah ya mchana asome kimyakimya. Isipokuwa tu swalah ya Fajr na swalah ya ijumaa.
Swali: Anataka kufanya marejeleo ya Qur-aan.
Jibu: Hapana. Sunnah ni kusoma kimyakimya. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akisoma kimyakimya katika swalah zinazopendeza za mchana.
Swali: Je, inafaa kwake kusoma kwa sauti ya juu akiswali na mwingine swalah ya mkusanyiko?
Jibu: Hapana, Sunnah ni yeye kusoma kimyakimya.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23074/حكم-رفع-الصوت-وخفضه-في-النوافل
- Imechapishwa: 02/11/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)