Swali: Wakati mwingine msafiri anafanya makisidio kuwa atafika katika mji wake katika swalah ya ´Ishaa.
Jibu: Ni sawa akiiswali safarini. Akiswali katika hali hiyo basi ataswali Rak´ah mbili. Na akisubiri mpaka atakapofika katika mji wake ataiswali Rak´ah nne.
Swali: Wakati mwingine wakati wanapofika katika vituo vya mafuta kabla ya kufikisha 80 km au chini ya 80 km wanaswali Maghrib pamoja na ´Ishaa kwa kukusanya na kufupisha.
Ibn Baaz: Ni wasafiri?
Muulizaji: Ndio.
Ibn Baaz: Hapana vibaya.
Muulizaji: 80 km?
Ibn Baaz: Hapana neno wakiswali kabla ya kufika katika mji wao. Kwa msemo mwingine wakiuacha mji wao.
Muulizaji: Hapana, ni kabla ya kuacha mji wao.
Ibn Baaz: Hapana. Kama hivo wataswali Rak´ah nne. Wakiacha miji yao ndio wataswali Rak´ah nne. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa anapoacha Madiynah ndipo anaswali Rak´ah mbili Dhul-Hulayfah.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23075/حكم-الجمع-والقصر-للمسافر-قبل-الوصول-للبلد
- Imechapishwa: 02/11/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)