Swali: Hadiyth ya ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) inasema kuwa wakati mwingine Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa analala akiwa na janaba na hagusi maji. Ni Swahiyh?
Jibu: Wameitia kasoro. Ina kasoro. Ni miongoni mwa mapokezi ya Abu Ishaaq as-Subay´iy na hakusema wazi amesimulia kutoka kwa nani. Kinachotambulika kutoka kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) baada ya kumjamii mke wake alikuwa akitawadha, akioga, akiosha dhakari yake, akitawadha na akilala. Wakati mwingine akitanguliza kuoga. Hakuwa akilala isipokuwa baada ya kutawadha, kama alivyomwambia ´Umar:
“Tawadha, kisha ndio ulale.”
Hapo ilikuwa pale ´Umar alipomwambia:
“Ee Mtume wa Allaah! Nilale nikiwa na janaba?” Akamjibu:
“Hapana, tawadha, kisha ndio ulale.”
Imekuja katika tamko jengine:
“Atawadhe na alale.”
Swali: Vipi ikiwa hatotawadha?
Jibu: Inachukiza.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Machukizo ya kulala na janaba bila kuoga
- Imechapishwa: 02/11/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)