Swali: Wako wanaofikiri kuwa kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni siku ya ijumaa peke yake.
Jibu: Hapana, ni kila wakati. Ni yenye kuenea. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
”Yule mwenye kuniswalia mara moja, basi Allaah atamswalia mara kumi.”[1]
Ni yenye kuenea katika nyakati zote; usiku na mchana, katika hali ya safari na hali ya ukazi, umeketi, umeegemea au unatembea. Ni kama mfano wa kumtaja Allaah. Ni aina fulani ya kumtaja Allaah.
Swali: Lakini inapendeza kumswalia kwa wingi siku ya ijumaa?
Jibu: Ataongeza zaidi. Kama mfano wa alivosema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
”Niswalieni kwa wingi siku ya ijumaa.”[2]
[1] Cheni ya wapokezi wake ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Fadhwl-us-Swalaah ´alaan-Nabiy” (08).
[2] Hadiyth ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Fadhwl-us-Swalaah ´alaan-Nabiy” (28).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23006/هل-فضل-الصلاة-والتسليم-يختص-بالجمعة
- Imechapishwa: 07/10/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)