Swali: Je, mtu anaweza kusema kuwa kutahiriwa ni wajibu?
Jibu: Haya ndio maoni ya kikosi kikubwa cha wanazuoni. Kwa sababu imepokelewa katika baadhi ya Hadiyth. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema wakati waliposilimu baadhi ya makafiri:
“Jiondoshe kikoi cha ukafiri na utahiri.”
Lakini kilichotangaa ni kwamba inapendeza. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwaamrisha watu wote wafanye jando. Kwa hiyo ikafahamisha kuwa ni jambo la kupendeza.
Swali: Je, mtu akiacha kutahiri si anakuwa amejifananisha na washirikina?
Jibu: Hapana, sio kujifananisha. Wako washirikina wanaofanya jando wakiwemo mayahudi.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22657/ما-الصحيح-في-حكم-الختان
- Imechapishwa: 15/07/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)