Swali: Maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Hakika yeye [ad-Dajjaal] ni chongo na hakika Mola wenu sio chongo.”
Je, kumethibitishwa macho mawili kwa Allaah?
Jibu: Ndio, kumethibitishwa macho mawili. Adiha kusikia na kuona zimetajwa ndani ya Qur-aan tukufu.
Swali: Ni kwa njia ya kipimo?
Jibu: Hapana, ni dalili ya wazi:
“… sio chongo.”
maana yake ni kwamba Mola wako ana macho mawili. ad-Dajjaal ana jicho moja na jicho jengine limefutika. Mola wako ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona, mpole, Mwenye huruma, anaghadhibika, anaridhika, anatoa na anazuia (´Azza wa Jall):
لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ۖوَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ
“Hakuna chochote kinachofanana Naye – Naye ni Mwenye kusikia yote, Mwenye kuona yote.”[1]
[1] 42:11
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22664/هل-في-حديث-ليس-باعور-اثبات-العينين-لله
- Imechapishwa: 15/07/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)