Imaam Ibn Qudaamah (Rahimahu Allaah) amesema:
Pepo na Moto vimeumbwa na havitotoweka. Pepo ni makazi ya wapenzi Wake na Moto ni adhabu ya maadui Wake. Watu wa Peponi watadumu humo milele
إِنَّ الْمُجْرِمِينَ فِي عَذَابِ جَهَنَّمَ خَالِدُونَ لَا يُفَتَّرُ عَنْهُمْ وَهُمْ فِيهِ مُبْلِسُونَ
”Hakika wahalifu wamo kwenye adhabu ya [Moto wa] Jahannam watadumu milele. Hawatopumzishwa nayo nao humo watakata tamaa.”[1]
MAELEZO
Pepo maana yake kilugha ni bustani yenye miti mingi. Pepo maana yake katika Shari´ah ni makazi ambayo Allaah ameyaandaa huko Aakhirah kwa ajili ya wenye kumcha.
Moto maana yake kilugha inatambulika. Moto maana yake katika Shari´ah ni makazi ambayo Allaah ameyaandaa huko Aakhirah kwa ajili ya makafiri.
Pepo na Moto tayari vimekwishaumbwa hivi sasa. Amesema (Ta´ala) kuhusu Pepo:
أُعِدَّتْ لِلْمُتَّقِينَ
“Imeandaliwa kwa wenye kumcha Allaah.”[2]
Amesema kuhusu Moto:
أُعِدَّتْ لِلْكَافِرِينَ
”Umeandaliwa kwa makafiri.”[3]
Maana ya kuandaliwa ni kutayarishwa.
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakati aliposwali swalah ya kupatwa kwa jua:
“Mimi nimeona Pepo na nikachukua kole la zabibu. Kama ningechukua makole mengi basi mgeyala muda wa kubakia dunia. Na nimeona Moto pia na sijapata kuona kitu cha kutisha sana kuliko hiyo.”[4]
Kuna maafikiano juu yake.
[1] 43:74-75
[2] 03:133
[3] 02:24
[4] al-Bukhaariy (1052) na Muslim (907, 17).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 131
- Imechapishwa: 05/12/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)