Uombezi huu unapingwa na Mu´tazilah na Khawaarij kutokana na ´Aqiydah yao kwamba watenda madhambi makubwa watadumishwa Motoni milele. Kwa hivyo wanaona kuwa hautowafaa uombezi. Tunawaraddi kwa yafuatayo:
1 – Hilo linaenda kinyume na Hadiyth tele zilizopokelewa kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
2 – Linaenda kinyume na maafikiano ya Salaf.
Uombezi una sharti mbili:
1 – Idhini ya Allaah kwa uombezi. Amesema (Ta´ala):
مَن ذَا الَّذِي يَشْفَعُ عِندَهُ إِلَّا بِإِذْنِهِ
“Nani huyu ambaye anashufai mbele Yake bila ya idhini Yake?”[1]
2 – Allaah ampe idhini mwenye kuombea na mwenye kuombewa. Amesema (Ta´ala):
وَلَا يَشْفَعُونَ إِلَّا لِمَنِ ارْتَضَىٰ
“Na wala hawamuombei uombezi yeyote yule isipokuwa yule Anayemridhia.”[2]
Kuhusu kafiri hana uombezi wowote. Amesema (Ta´ala):
فَمَا تَنفَعُهُمْ شَفَاعَةُ الشَّافِعِينَ
“Basi haitowafaa uombezi wowote wa waombezi.”[3]
Bi maana tutakadiria mtu kuwaombea basi hautowafaa kitu uombezi wao.
[1] 02:255
[2] 21:28
[3] 74:48
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 130
- Imechapishwa: 06/12/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)