Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Mfano wa aina za ´ibaadah ambazo Allaah ameamrisha ni Uislamu, Imani na Ihsaan.
MAELEZO
Shaykh (Rahimahu Allaah) ameleta mifano ya ´ibaadah kwa njia ya kupigia mfano na si kwa njia ya ufupikaji. Kwa sababu ni zaidi ya alizotaja. Haiwezekani kuziorodhesha katika kujitabu kidogo. Lakini ameleta mifano tu. Shaykh-ul-Islaam ana kitabu cha kujitegemea kwa jina “al-´Ubuudiyyah” kinachotafiti mambo ya ´ibaadah, aina zake na ubainifu wa upondokaji uliyofanywa na Suufiyyah na wengineo katika ´ibaadah. Ni kitabu muhimu ambacho mwanafunzi anahitajia kukisoma. Maneno yake (Rahimahu Allaah):
“Mfano wa Uislamu, imani na Ihsaan.”
Haya matatu ndio aina kubwa za ´ibaadah; Uislamu, imani na ihsaan. Maelezo yake yatakuja katika maneno ya Shaykh (Rahimahu Allaah) katika msingi wa pili. Ameyataja hapa kwa sababu ni miongoni mwa aina za ´ibaadah.
Uislamu kwa nguzo zake tano: shahaadah, kusimamisha swalah, kutoa zakaah, kufunga Ramadhaan na kuhiji nyumba tukufu ya Allaah. Yote haya ni ´ibaadah za kimwili na za kimali.
Vivyo hivyo nguzo sita za imani: kumwamini Allaah, Malaika Wake, Vitabu Vyake, Mitume Yake, siku ya Mwisho na kuamini Qadar kheri na shari yake. Hizi ni ´ibaadah za kimoyo.
Vivyo hivyo Ihsaan ambayo ina nguzo moja: Kumwabudu Allaah kama vile unamuona na ikiwa wewe humuoni basi tambua kuwa Yeye anakuona. Hii ndio ´ibaadah iliyo juu zaidi. Kwa sababu Ihsaan ndio aina ya juu kabisa ya ´ibaadah.
Mambo haya ndio huitwa ngazi za dini. Kwa sababu mkusanyiko wa yote hayo ndio dini. Kwa sababu Jibriyl alipomuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mbele ya Maswahabah zake baada ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumjibu juu ya Uislamu, imani na Ihsaan akasema:
“Huyu ni Jibriyl. Amekujieni kukufunzeni jambo la dini yenu.”[1]
Kwa hiyo mambo haya matatu yakaitwa ndio dini.
[1] al-Bukhaariy (4777) na Muslim (08, 09 na 10).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 124-127
- Imechapishwa: 23/12/2020
Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Mfano wa aina za ´ibaadah ambazo Allaah ameamrisha ni Uislamu, Imani na Ihsaan.
MAELEZO
Shaykh (Rahimahu Allaah) ameleta mifano ya ´ibaadah kwa njia ya kupigia mfano na si kwa njia ya ufupikaji. Kwa sababu ni zaidi ya alizotaja. Haiwezekani kuziorodhesha katika kujitabu kidogo. Lakini ameleta mifano tu. Shaykh-ul-Islaam ana kitabu cha kujitegemea kwa jina “al-´Ubuudiyyah” kinachotafiti mambo ya ´ibaadah, aina zake na ubainifu wa upondokaji uliyofanywa na Suufiyyah na wengineo katika ´ibaadah. Ni kitabu muhimu ambacho mwanafunzi anahitajia kukisoma. Maneno yake (Rahimahu Allaah):
“Mfano wa Uislamu, imani na Ihsaan.”
Haya matatu ndio aina kubwa za ´ibaadah; Uislamu, imani na ihsaan. Maelezo yake yatakuja katika maneno ya Shaykh (Rahimahu Allaah) katika msingi wa pili. Ameyataja hapa kwa sababu ni miongoni mwa aina za ´ibaadah.
Uislamu kwa nguzo zake tano: shahaadah, kusimamisha swalah, kutoa zakaah, kufunga Ramadhaan na kuhiji nyumba tukufu ya Allaah. Yote haya ni ´ibaadah za kimwili na za kimali.
Vivyo hivyo nguzo sita za imani: kumwamini Allaah, Malaika Wake, Vitabu Vyake, Mitume Yake, siku ya Mwisho na kuamini Qadar kheri na shari yake. Hizi ni ´ibaadah za kimoyo.
Vivyo hivyo Ihsaan ambayo ina nguzo moja: Kumwabudu Allaah kama vile unamuona na ikiwa wewe humuoni basi tambua kuwa Yeye anakuona. Hii ndio ´ibaadah iliyo juu zaidi. Kwa sababu Ihsaan ndio aina ya juu kabisa ya ´ibaadah.
Mambo haya ndio huitwa ngazi za dini. Kwa sababu mkusanyiko wa yote hayo ndio dini. Kwa sababu Jibriyl alipomuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mbele ya Maswahabah zake baada ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumjibu juu ya Uislamu, imani na Ihsaan akasema:
“Huyu ni Jibriyl. Amekujieni kukufunzeni jambo la dini yenu.”[1]
Kwa hiyo mambo haya matatu yakaitwa ndio dini.
[1] al-Bukhaariy (4777) na Muslim (08, 09 na 10).
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 124-127
Imechapishwa: 23/12/2020
https://firqatunnajia.com/58-mfano-wa-aina-za-ibaadah-alizoamrisha-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)