41 – Ismaa´iyl bin Abiy Uways ametuhadithia: Sulaymaan bin Bilaal ametuhadithia, kutoka kwa Ja´far, kutoka kwa baba yake, ambaye ameeleza kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
من ينسى الصلاة عليَّ خطئ أبواب الجنة
”Yule mwenye kuacha kuniswalia, basi atapotea kutokamana na milango ya Pepo.”[1]
[1] Cheni ya wapokezi wake ni nzuri, lakini kuna Swahabah anayekosekana. Ja´far anaitwa Ja´far bin Muhammad bin ´Aliy bin al-Husayn bin ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anhum). Baba yake Muhamamd anajulikana kama Abu Ja´far al-Baaqir. Mtunzi wa kitabu ataipokea kupitia njia mbili zitazokuja huko mbele kutoka kwake, lakini hali ya kukosekana Swahabah. Hata hivyo at-Twabaraaniy ameiunganisha katika “al-Mu´jam al-Kabiyr” (1/139/1) kupitia kwa Muhammad bin Bashiyr al-Kindiy: ´Ubaydah bin Humayd ametuhadithia: Fitwr bin Khaliyfah amenihadithia, kutoka kwa Abu Ja´far Muhammad bin ´Aliy bin al-Husayn, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa baba yake, ambaye amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema… Kwa mujibu wa ad-Daaraqutwniy al-Kindiy si mwenye nguvu katika masimulizi yake, kwa ajili hiyo hakuzingatiwi kule kukhalifu kwake. Pengine ndio maana al-Mundhiriy akasema kuwa kuwa Hadiyth inafanana zaidi na ambayo kuna Swahabah aliyekosekana katika cheni ya wapokezi. Hata hivyo Hadiyth inatiliwa nguvu na upokezi wa Ibn ´Abbaas kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ameipokea Ibn Maajah (908) na upokezi wa Muhammad bin al-Hanafiyyah kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ibn Abiy ´Aaswim ameipokea hali ya kukosekana Swahabah katika cheni ya wapokezi. Hata kama njia zote hizi zina udhaifu, lakini zinapeana nguvu. Kwa ajili hiyo Hadiyth angalau kwa uchache kabisa ni nzuri.
- Mhusika: Imaam Ismaa´iyl bin Ishaaq al-Maalikiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fadhwl-us-Swalaah ´alaan-Nabiy, uk. 46-47
- Imechapishwa: 16/01/2024
- taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
41 – Ismaa´iyl bin Abiy Uways ametuhadithia: Sulaymaan bin Bilaal ametuhadithia, kutoka kwa Ja´far, kutoka kwa baba yake, ambaye ameeleza kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
من ينسى الصلاة عليَّ خطئ أبواب الجنة
”Yule mwenye kuacha kuniswalia, basi atapotea kutokamana na milango ya Pepo.”[1]
[1] Cheni ya wapokezi wake ni nzuri, lakini kuna Swahabah anayekosekana. Ja´far anaitwa Ja´far bin Muhammad bin ´Aliy bin al-Husayn bin ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anhum). Baba yake Muhamamd anajulikana kama Abu Ja´far al-Baaqir. Mtunzi wa kitabu ataipokea kupitia njia mbili zitazokuja huko mbele kutoka kwake, lakini hali ya kukosekana Swahabah. Hata hivyo at-Twabaraaniy ameiunganisha katika “al-Mu´jam al-Kabiyr” (1/139/1) kupitia kwa Muhammad bin Bashiyr al-Kindiy: ´Ubaydah bin Humayd ametuhadithia: Fitwr bin Khaliyfah amenihadithia, kutoka kwa Abu Ja´far Muhammad bin ´Aliy bin al-Husayn, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa baba yake, ambaye amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema… Kwa mujibu wa ad-Daaraqutwniy al-Kindiy si mwenye nguvu katika masimulizi yake, kwa ajili hiyo hakuzingatiwi kule kukhalifu kwake. Pengine ndio maana al-Mundhiriy akasema kuwa kuwa Hadiyth inafanana zaidi na ambayo kuna Swahabah aliyekosekana katika cheni ya wapokezi. Hata hivyo Hadiyth inatiliwa nguvu na upokezi wa Ibn ´Abbaas kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ameipokea Ibn Maajah (908) na upokezi wa Muhammad bin al-Hanafiyyah kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ibn Abiy ´Aaswim ameipokea hali ya kukosekana Swahabah katika cheni ya wapokezi. Hata kama njia zote hizi zina udhaifu, lakini zinapeana nguvu. Kwa ajili hiyo Hadiyth angalau kwa uchache kabisa ni nzuri.
Mhusika: Imaam Ismaa´iyl bin Ishaaq al-Maalikiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fadhwl-us-Swalaah ´alaan-Nabiy, uk. 46-47
Imechapishwa: 16/01/2024
taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
https://firqatunnajia.com/41-hadiyth-yule-mwenye-kuacha-kuniswalia/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)