172 – Maalik bin Anas amesema:
“Ambaye atalazimiana na Sunnah na wakasalimika naye Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kisha akafa, basi atakuwa pamoja na Mitume, wakweli mno, mashahidi na waja wema, hata kama atafanya upungufu katika matendo.”
Bishr bin al-Haarith amesema:
“Uislamu ni Sunnah na Sunnah ni Uislamu.”
Fudhwayl bin ´Iyaadhw amesema:
“Pindi ninapomuona mtu katika Ahl-us-Sunnah, nahisi ni kama kwamba nimemuona mmoja katika Maswahabah wa Allaah wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Pindi ninapomuona mtu katika Ahl-ul-Bid´ah, nahisi ni kama kwamba nimemuona mmoja katika wanafiki.”
Yuunus bin ´Ubayd amesema:
“Ajabu ni kwa yule ambaye leo analingania katika Sunnah. Ajabu zaidi ni kwa yule anayeitikia na kuikubali Sunnah.”[1]
Ibn ´Awn alikuwa akisema wakati wa kukata roho mpaka alipokata roho:
“Ala ala Sunnah! Ala ala Sunnah! Na tahadharini na Bid´ah.”
Ahmad bin Hanbal amesema:
“Mmoja katika wenzangu alifariki na akaonekana ndotoni akisema: “Mwambieni Abu ´Abdillaah: “Jilazimishe na Sunnah!”, kwani hakika kitu cha kwanza alichoniuliza Allaah ni juu ya Sunnah.””
Abul-´Aaliyah amesema:
“Mwenye kufa juu ya Sunnah katika hali ya kusitiriwa, huyo ni mkweli. Kunasemwa kwamba ushikamana na Sunnah ni kuokoka.”
Sufyaan ath-Thawriy amesema:
“Mwenye kumtegea sikio yake mtu wa Bid´ah, basi ametoka katika ulinzi wa Allaah na ametegemezwa mwenyewe kwayo.”
Kwa maana kwa Bid´ah.”
Abu Daawuud bin Abiy Hind amesema:
“Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) alimfunulia wahy Muusa bin ´Imraan: “Usikae na Ahl-ul-Bid´ah. Ukikaa nao na kukapenyeza ndani ya moyo wako kitu katika yale wanayoyasema, Nitakutupa Motoni.””[2]
[1] Abu Nu´aym (03/21), Ibn Battwah katika “al-Ibaanah al-Kubraa” (20) na wengineo.
[2] Ibn Wadhdhwaah katika “al-Bid´ah”, uk. 49.
- Mhusika: Imaam Abu Muhammad al-Hasan bin Khalaf al-Barbahaariy (kfk. 329)
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh-us-Sunnah, uk. 136-138
- Imechapishwa: 30/12/2024
172 – Maalik bin Anas amesema:
“Ambaye atalazimiana na Sunnah na wakasalimika naye Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kisha akafa, basi atakuwa pamoja na Mitume, wakweli mno, mashahidi na waja wema, hata kama atafanya upungufu katika matendo.”
Bishr bin al-Haarith amesema:
“Uislamu ni Sunnah na Sunnah ni Uislamu.”
Fudhwayl bin ´Iyaadhw amesema:
“Pindi ninapomuona mtu katika Ahl-us-Sunnah, nahisi ni kama kwamba nimemuona mmoja katika Maswahabah wa Allaah wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Pindi ninapomuona mtu katika Ahl-ul-Bid´ah, nahisi ni kama kwamba nimemuona mmoja katika wanafiki.”
Yuunus bin ´Ubayd amesema:
“Ajabu ni kwa yule ambaye leo analingania katika Sunnah. Ajabu zaidi ni kwa yule anayeitikia na kuikubali Sunnah.”[1]
Ibn ´Awn alikuwa akisema wakati wa kukata roho mpaka alipokata roho:
“Ala ala Sunnah! Ala ala Sunnah! Na tahadharini na Bid´ah.”
Ahmad bin Hanbal amesema:
“Mmoja katika wenzangu alifariki na akaonekana ndotoni akisema: “Mwambieni Abu ´Abdillaah: “Jilazimishe na Sunnah!”, kwani hakika kitu cha kwanza alichoniuliza Allaah ni juu ya Sunnah.””
Abul-´Aaliyah amesema:
“Mwenye kufa juu ya Sunnah katika hali ya kusitiriwa, huyo ni mkweli. Kunasemwa kwamba ushikamana na Sunnah ni kuokoka.”
Sufyaan ath-Thawriy amesema:
“Mwenye kumtegea sikio yake mtu wa Bid´ah, basi ametoka katika ulinzi wa Allaah na ametegemezwa mwenyewe kwayo.”
Kwa maana kwa Bid´ah.”
Abu Daawuud bin Abiy Hind amesema:
“Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) alimfunulia wahy Muusa bin ´Imraan: “Usikae na Ahl-ul-Bid´ah. Ukikaa nao na kukapenyeza ndani ya moyo wako kitu katika yale wanayoyasema, Nitakutupa Motoni.””[2]
[1] Abu Nu´aym (03/21), Ibn Battwah katika “al-Ibaanah al-Kubraa” (20) na wengineo.
[2] Ibn Wadhdhwaah katika “al-Bid´ah”, uk. 49.
Mhusika: Imaam Abu Muhammad al-Hasan bin Khalaf al-Barbahaariy (kfk. 329)
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh-us-Sunnah, uk. 136-138
Imechapishwa: 30/12/2024
https://firqatunnajia.com/35-amekosa-hekima/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)