Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema:
“Kuchukulia uvaaji wa vazi la pamba ni ´ibaadah na kujikurubisha kwa Allaah ni Bid´ah.”[1]
Kwa msemo mwingine imethibiti kuwa Bid´ah zinaingia katika mambo ya kiada kama ambavo zinaingia katika mambo ya ´ibaadah. Inafaa kuacha kula nyama, lakini mtu akiacha kula nyama kwa lengo la ´ibaadahbasi kitendo chake kinakuwa Bid´ah. ash-Shaatwibiy amesema:
“Bid´ah inatokea pale tu ambapo mzushi atafanya kitendo cha halali kwa kuamini kuwa kimewekwa katika Shari´ah ilihali ukweli wa mambo hakikuwekwa katika Shari´ah.”[2]
Vivyo hivyo kuvaa nguo kwa rangi maalum ni kitu kilichohalalishwa; lakini akivaa nguo ya rangi maalum kwa lengo la ´ibaadah inakuwa ni Bid´ah yenye kuchukiwa.
[1]Majmuu´-ul-Fataawaa (11/555).
[2] al-I´tiswaam.
- Mhusika: Shaykh ´Abdus-Salaam bin Barjas Aal ´Abdil-Kariym
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Hujaj al-Qawiyyah ´alaa anna Wasaa-il-ad-Da´wah Tawqiyfiyyah, uk. 30
- Imechapishwa: 10/05/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)