Himdi zote njema anastahiki Allaah. Swalah na amani zimwendee Mtume wa Allaah, kizazi chake na Maswahabah zake wote.
Ama baada ya hayo;
Miongoni mwa wepesi wa Shari´ah ni zile ruhusa zilizokuja za swawm. Miongoni mwazo:
1 – Mwenye kula au kunywa kwa kusahau basi funga yake ni sahihi. Hatolazimika kulipa kwa mujibu wa maoni sahihi zaidi ya wanazuoni. Imethibiti kwa al-Bukhaariy na Muslim waliopokea kupitia kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye amesimulia kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Akisahau ambapo akala na kunywa, basi akamilishe funga yake. Hakika hapana vyenginevyo Allaah ndiye kamilisha na kumnywesha.”[1]
Tamko la Muslim linasema:
“Mwenye kusahau hali ya kuwa amefunga ambapo akala na kunywa, basi akamilishe swawm yake. Hakika si vyenginevyo Allaah ndiye kamlisha na kumnywesha.”[2]
Yale yaliyofahamishwa na Hadiyth kwamba aliyesahau sio wajibu kwake kulipa ndio maoni ya sawa ambayo wameenda kwayo kikosi cha wanazuoni wengi.
[1] al-Bukhaariy (1933) na Muslim (1155).
[2] Muslim (1155).
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Duruus fiy Ramadhwaan, uk. 42
- Imechapishwa: 19/04/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)