Miongoni mwa dalili zinazofahamisha kupendeza kuharakisha kukata swawm:
1 – Imethibiti kwa al-Bukhaariy na Muslim waliopokea kupitia kwa ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Usiku ukija hapa [mashariki] na ukaondoka mchana hapa [magharibi] na likazama jua, basi amekwishafungua mfungaji.”[1]
2 – Kuchelewesha daku. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَكُلُوا وَاشْرَبُوا حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَكُمُ الْخَيْطُ الْأَبْيَضُ مِنَ الْخَيْطِ الْأَسْوَدِ مِنَ الْفَجْرِ اللَّيْلِ
“Kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa alfajiri katika weusi wa usiku.”[2]
Vilevile imethibiti kwa al-Bukhaariy na Muslim waliopokea kupitia kwa Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ambaye amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika Bilaal anaadhini usiku. Hivyo kuleni na kunyweni mpaka aadhini Ibn Umm Maktuum.”
al-Qaasim bin Muhammad – mmoja katika wasimuliaji wa Hadiyth hiyo – amesema:
“Kitambo kilichokuwepo kati yake [daku na adhaana] ni kupanda kwa huyu na kushuka kwa huyu.”[3]
Miongoni mwa dalili zinazofahamisha kupendeza kwa daku ni yale yaliyothibiti kwa al-Bukhaariy na Muslim waliopokea kupitia kwa Anas (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kuleni daku. Kwani hakika katika kula daku kuna baraka.”[4]
3 – Inapendeza kuchelewesha daku kutokana na yaliyothibiti kwa al-Bukhaariy na Muslim waliopokea kupitia kwa Yaziyd bin Thaabit (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye amesimulia:
“Tulikula daku pamoja na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kisha akasimama kuswali.”Nikauliza: “Kulikuwa na kitambo gani kati ya adhaana na daku?”Akasema: “Kiasi cha Aayah khamsini.”[5]
Allaah awawafikishe wote kumtii, awaruzuku wote elimu yenye manufaa na matendo mema.
Swalah na amani zimwendee Mtume wa Allaah, kizazi chake na Maswahabah zake wote.
[1] al-Bukhaariy (1954) na Muslim (1100).
[2] 02:187
[3] al-Bukhaariy (617) na Muslim (1092).
[4] al-Bukhaariy (1923) na Muslim (1095).
[5] al-Bukhaariy (1921) na Muslim (1097).
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Duruus fiy Ramadhwaan, uk. 40-41
- Imechapishwa: 19/04/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)