82 – Muhammad amesema: Abu ´Umar adh-Dhwariyr ametuhadithia: al-Hasan bin Diynaar ametuhadithia, kutoka kwa al-Hasan, ambaye amesema:
”Hapo kitambo ilikuwa ni aibu kwa muislamu kuambiwa kuwa wewe ni mnene.”
83 – Muhammad amesema: ´Ubaydullaah bin Muhammad at-Taymiy ametuhadithia: Salamah bin Sa´iyd ametuhadithia:
”Mtu alikuwa anaweza kusemwa vibaya kwa unene kama anavosemwa vibaya kwa dhambi aliyofanya.”
84 – Nimehadithiwa kutoka kwa al-Mu´aafaa bin ´Imraan, kutoka kwa Sufyaan ath-Thawriy, kutoka kwa ´Amr bin Qays al-Malaa-iy, ambaye amesema:
”Jihadharini na unene. Hakika unaufanya moyo kuwa mgumu.”
85 – al-Husayn bin ´Abdir-Rahmaan amenihadithia: Baadhi ya wanazuoni wamesema:
”Ikiwa wewe ni mnene, basi jizingatie kuwa mgonjwa mpaka pale utakapopungua.”
86 – Ameeleza tena kuwa Ibn-ul-A´raabiy amesema:
”Waarabu walikuwa wakiona kuwa mtu halali akiwa ni mnene akawa ni mwenye maamuzi.”
87 – Abu Haatim ar-Raaziy amenihadithia, kutoka kwa Ahmad bin Abiyl-Hawaariy: Abu Sulaymaan amesema:
”Unapotaka kufanya jambo miongoni mwa mambo ya kidunia na Aakhirah, basi usile mpaka umelifanya. Kwani hakika kula kunaibadilisha akili.”
88 – ´Aliy bin Ja´far al-Ahmar amesema: Nimemsikia baba yangu akisema kuwa Ayyuub alikuwa akisema:
”Kula sana ni maradhi ya tumbo na ni kuzidi kuoza.”
- Muhusika: Imaam Abu Bakr ´Abdullaah bin Muhammad bin Abiyd-Dunyaa
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kitaab-ul-Juu´, uk. 72-74
- Imechapishwa: 20/06/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)