Swali: Katika kijiji chetu watu wanasoma katika swalah ya kisimamo cha usiku katika Ramadhaan Suurah “al-Ikhlaasw”, pamoja na “Subhaan Allaah”, “Alhamdulillaah”, “Allaahu Akbar” na “Laa hawlah wa laa quwwatah illaa billaah al-´Adhwiym” kwa pamoja kila baada ya Rak´ah mbili kwa kunyanyua sauti, jambo ambalo linaondosha utulivu. Je, kusema hivi Sunnah yoyote takasifu?
Jibu: Kitendo hichi ni Bid´ah na haifai kukifanya. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yeyote mwenye kuzua katika dini yetu hii kisichokuwemo basi atarudishiwa mwenyewe.”[1]
Kuna maafikiano juu ya usahihi wake.
“Yeyote atakayefanya kitendo kisichoafikiana na amri yetu atarudishiwa mwenyewe.”[2]
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema katika Khutbah ya ijumaa:
“Amma bad´; hakika mazungumzo bora ni Kitabu cha Allaah, mwongozo bora ni wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), shari ya mambo ni yale yenye kuzuliwa na kila chenye kuzuliwa ni Bid´ah.”[3]
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Kitendo hichi ni Bid´ah ambacho hakikufanywa na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wala Maswahabah zake (Radhiya Allaahu ´anhum). Kwa hiyo ni wajibu kuyaacha na kutubu kwa Allaah (Subhaanah) kwa yale yaliyotangulia. Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
وَتُوبُوا إِلَى اللَّـهِ جَمِيعًا أَيُّهَ الْمُؤْمِنُونَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ
“Tubuni kwa Allaah nyote, enyi waumini, mpate kufaulu.”[4]
وَإِنِّي لَغَفَّارٌ لِّمَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ صَالِحًا ثُمَّ اهْتَدَىٰ
”Hakika Mimi ni Mwingi mno wa kusamehe kwa anayetubia na akaamini na akatenda mema kisha akaendelea kuongoka.”[5]
[1] al-Bukhaariy (2697), Muslim (1718), Abu Daawuud (4606), Ibn Maajah (14) na Ahmad (06/256).
[2] Muslim (1718).
[3] Muslim (867), an-Nasaa´iy (1578), Ahmad (03/371) na ad-Daarimiy (206).
[4] 24:31
[5] 20:82
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/44-46)
- Imechapishwa: 11/09/2021
Swali: Katika kijiji chetu watu wanasoma katika swalah ya kisimamo cha usiku katika Ramadhaan Suurah “al-Ikhlaasw”, pamoja na “Subhaan Allaah”, “Alhamdulillaah”, “Allaahu Akbar” na “Laa hawlah wa laa quwwatah illaa billaah al-´Adhwiym” kwa pamoja kila baada ya Rak´ah mbili kwa kunyanyua sauti, jambo ambalo linaondosha utulivu. Je, kusema hivi Sunnah yoyote takasifu?
Jibu: Kitendo hichi ni Bid´ah na haifai kukifanya. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yeyote mwenye kuzua katika dini yetu hii kisichokuwemo basi atarudishiwa mwenyewe.”[1]
Kuna maafikiano juu ya usahihi wake.
“Yeyote atakayefanya kitendo kisichoafikiana na amri yetu atarudishiwa mwenyewe.”[2]
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema katika Khutbah ya ijumaa:
“Amma bad´; hakika mazungumzo bora ni Kitabu cha Allaah, mwongozo bora ni wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), shari ya mambo ni yale yenye kuzuliwa na kila chenye kuzuliwa ni Bid´ah.”[3]
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Kitendo hichi ni Bid´ah ambacho hakikufanywa na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wala Maswahabah zake (Radhiya Allaahu ´anhum). Kwa hiyo ni wajibu kuyaacha na kutubu kwa Allaah (Subhaanah) kwa yale yaliyotangulia. Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
وَتُوبُوا إِلَى اللَّـهِ جَمِيعًا أَيُّهَ الْمُؤْمِنُونَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ
“Tubuni kwa Allaah nyote, enyi waumini, mpate kufaulu.”[4]
وَإِنِّي لَغَفَّارٌ لِّمَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ صَالِحًا ثُمَّ اهْتَدَىٰ
”Hakika Mimi ni Mwingi mno wa kusamehe kwa anayetubia na akaamini na akatenda mema kisha akaendelea kuongoka.”[5]
[1] al-Bukhaariy (2697), Muslim (1718), Abu Daawuud (4606), Ibn Maajah (14) na Ahmad (06/256).
[2] Muslim (1718).
[3] Muslim (867), an-Nasaa´iy (1578), Ahmad (03/371) na ad-Daarimiy (206).
[4] 24:31
[5] 20:82
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/44-46)
Imechapishwa: 11/09/2021
https://firqatunnajia.com/duaa-za-pamoja-kila-baada-ya-rakaa-mbili-za-tarawiyh/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)