Swali: Anayekula mchana wa Ramadhaan kutokana na udhuru, kama vile safari au ugonjwa, na baadaye udhuru wake ukaondoka. Je, atatakiwa kuendelea kula na kunywa au atajizuilia?
Jibu: Analazimika kujizuilia siku yake iliyobaki kwa sababu ni miongoni mwa watu walioshuhudia mwezi. Baadaye atalipa siku hiyo kwa sababu hakufunga siku nzima. Anaingia ndani ya maneno Yake Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala):
فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ
“Basi atakayeshuhudia miongoni mwenu mwezi mpya na afunge na atakayekuwa mgonjwa au safarini, basi atimize idadi katika masiku mengine.”[1]
[1] 02:185
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah Aalush-Shaykh
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Min Fataawaas-Swiyaam, uk. 20
- Imechapishwa: 20/03/2022
Swali: Anayekula mchana wa Ramadhaan kutokana na udhuru, kama vile safari au ugonjwa, na baadaye udhuru wake ukaondoka. Je, atatakiwa kuendelea kula na kunywa au atajizuilia?
Jibu: Analazimika kujizuilia siku yake iliyobaki kwa sababu ni miongoni mwa watu walioshuhudia mwezi. Baadaye atalipa siku hiyo kwa sababu hakufunga siku nzima. Anaingia ndani ya maneno Yake Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala):
فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ
“Basi atakayeshuhudia miongoni mwenu mwezi mpya na afunge na atakayekuwa mgonjwa au safarini, basi atimize idadi katika masiku mengine.”[1]
[1] 02:185
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah Aalush-Shaykh
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Min Fataawaas-Swiyaam, uk. 20
Imechapishwa: 20/03/2022
https://firqatunnajia.com/14-kile-kilichokuwa-kinamruhusu-kutofunga-kimeondoka-wakati-wa-mchana/