41 – Khaalid bin Khidaash ametuhadithia: al-Mu´allaa al-Warraaq ametuhadithia: Nilimsikia Maalik bin Diynaar akisema:
”Nilichanganya unga wangu na majivu na nikadhoofika kutokana na swalah. Ningelikuwa na nguvu ya kuswali basi nisingekula chakula kingine zaidi yake.”
42 – Khaalid ametuhadithia: al-Mu´allaa al-Warraaq ametuhadithia: Abu ´Ubaydah al-Khawwaasw amesema:
”Kifo chako kiko katika shibe yako na bahati yako iko katika njaa yako. Ikiwa umeshiba [tupu] na ukalala, basi adui anaweza kumakinika kwako. Lakini unapokuwa na njaa, basi unakuwa makini juu ya adui.”
43 – ´Abdullaah bin ´Iysaa at-Twafaawiy ametuhadithia: ´Abdullaah ash-Shahhaam ametuhadithia: Maalik bin Diynaar amesema:
”Kwa muda wa asubuhi arobaini nilikula chakula cha kubana. Isingekuwa kwamba nachelea kudhoofika, basi ningelazimiana na jambo hilo.”
44 – Muhammad bin ´Umar bin ´Aliy al-Muqaddimiy amenihadithia: Nilimsikia Yuusuf bin ´Atwiyyah bin Baab as-Swaffaar: Nilimsikia Maalik bin Diynaar akisema:
”Ingelikuwa majivu yanaingia kooni mwangu, basi ningeyala.”
45 – Haaruun bin ´Abdillaah ametuhadithia: Sayyaar ametuhadithia: ´Uthmaan bin Ibraahiym, mmoja katika marafiki zake Maalik bin Diynaar, ametuhadithia:
”Nilimsikia Maalik akimwambia mmoja katika ndugu zake: ”Natamani mkate laini na mnene kwa mtindi.” Bwana yule akaondoka na kumletea navyo. Akawa akavitazama na kusema: ”Mimi nimekutamani tangu miaka arobaini iliyopita na daima nimekushinda – unataka kunishinda hivi sasa? Viondoshe hapa kwangu.” Akakataa kuvila.
46 – Muhammad bin al-Husayn amesema: Khaalid bin Yaziyd at-Twabiyb ametuhadithia: Khaazim bin al-Husayn ametuhadithia: Nilimsikia Maalik bin Diynaar akisema:
”Unalipenda tumbo lako zaidi kuliko dini yako? Je, unalitanguliza mbele tumbo lako kuliko nafsi yako? Hebu wazia umelijaza chakula kizuri na kinywaji kitamu zaidi – tazama ni nini [tupu].”
47 – Haaruun bin ´Abdillaah ametuhadithia: Sayyaar ametuhadithia: Ja´far ametuhadithia: Nilimsikia Maalik bin Diynaar akisema:
”Ni nani yuko katika kikao chenu hiki? Naapa kwa Allaah! Hapo sijaonja tende ambayo haijakomaa, tende tosa wala tende kavu. Ni kipi kimepungua kwangu na kukunyanyueni nyinyi?”
48 – Muhammad bin al-Husayn ametuhadithia: Daawuud bin Muhabbar ametuhadithia: ´Abdul-Waahid bin Ziyaad ametuhadithia: Nilimsikia Maalik akimwambia Hawshab:
”Ee Abu Bishr! Yahifadhi kutoka kwangu mambo mawili: usilale hali ya kuwa umeshiba na kiache chakula hali ya kuwa unakitamani.” Hawshab akasema: ”Ee Abu Yahyaa! Hayo ni maelekezo ya mapishi ya madaktari wa ulimwenguni.” Muhammad bin Waasiy´ akayasikia maneno yao akasema: ”Ndio, na ni maelekezo ya mapishi ya njia ya kwenda Aakhirah.” Ndipo Maalik akasema: ”Hapana, ni ya Aakhirah na ulimwenguni.”
- Muhusika: Imaam Abu Bakr ´Abdullaah bin Muhammad bin Abiyd-Dunyaa
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kitaab-ul-Juu´, uk. 54-56
- Imechapishwa: 19/06/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)