Zipo Aayah na Hadiyth nyingi zilizopokelewa kuhusu ubora wa ulinganizi na walinganizi. Ni kama ambavo kumepokelewa Hadiyth nyingi zinazotambulika kwa wanazuoni juu ya kitendo cha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuwatuma walinganizi. Miongoni mwazo ni maneno Yake (Jalla wa ´Alaa):
وَمَنْ أَحْسَنُ قَوْلًا مِّمَّن دَعَا إِلَى اللَّهِ وَعَمِلَ صَالِحًا وَقَالَ إِنَّنِي مِنَ الْمُسْلِمِينَ
“Na nani mwenye kauli nzuri zaidi kuliko yule anayelingania watu kwa Allaah na akatenda mema na akasema: “Hakika mimi ni miongoni mwa waislamu?”[1]
Aayah hii tukufu inawasifia walinganizi na kwamba hakuna yeyote ambaye ana maneno mazuri kuwashinda wao. Katika kilele chao wako Mitume (Swalla Allaahu ´alayhim wa sallam). Kisha wafuasi wao kutegemea daraja zao katika kulingania, elimu na ubora. Wewe, ee mja wa Allaah, inakutosha kuwa utukufu kwa kuwa ni miongoni mwa wafuasi wa Mitume.
[1] 41:33
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ad-Da´wah ilaa Allaah wa Akhlaaq-id-Du´aah, uk. 20-21
- Imechapishwa: 04/06/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)