Unapowafundisha wengine elimu na ukaisambaza kwa watu unalipwa thawabu kwa njia nyingi:
1 – Kueneza kwako elimu unaeneza dini ya Allaah (´Azza wa Jall). Hivyo unakuwa katika wapambanaji jihaad katika njia ya Allaah, kwani unazifungua nyoyo kwa elimu kama ambavyo wapiganaji jihaad wanaifungua miji kwa silaha na imani.
2 – Miongoni mwa baraka za kueneza elimu na kuifundisha ndani yake kuna kuihifadhi na kuilinda Shari´ah ya Allaah (´Azza wa Jall), kwa sababu Shari´ah haihifadhiki bila ya elimu.
3 – Miongoni mwa baraka za kueneza elimu ni kwamba unamtendea wema huyu ambaye umemfunza, kwa sababu unamfanya kuifahamu dini ya Allaah (´Azza wa Jall). Akimwabudu Allaah kwa ujuzi basi unalipwa sawa na thawabu zake, kwa sababu wewe ndiye ambaye umemwongoza katika kheri hiyo. Mwenye kuongoza katika kheri ni kama mwenye kuitenda.
4 – Kueneza elimu na kuifundisha kunaifanya inazidi. Elimu ya mwanachuoni inazidi akiwasomesha watu. Kwa sababu ni kujikumbusha yale aliyohifadhi na kuyafungua yale ambayo hakuyahifadhi. Kama alivosema msemaji:
يزيد بكثرة الإنفاق منه
Inazidi kwa kuitoa kwa wingi
وينقص إن به كفا شددتا
Na inapungua kwa kuizuia
Bi maana inapungua kwa kule kuizuia na kutoifunza.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Du´aa´ al-Qunuut-il-Witr, uk. 12-13
- Imechapishwa: 09/03/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)