20 – Muhammad bin Yahyaa bin ´Abdillaah ametukhabarisha: Ya´quub bin Ibraahiym ametukhabarisha: Baba yangu ametukhabarisha, kutoka kwa Swaalih, kutoka kwa Ibn Shihaab: Abu Umaamah bin Sahl amenihadithia ambaye amehadithia kuwa amemsikia Abu Sa´iyd al-Khudriy akisimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema:

”Wakati nilipokuwa nimelala niliota watu wakiwa wamevaa makanzu marefu. Kuna zilizokuwa zinafika kifuani, zingine zinafika chini ya hapo.” ´Umar bin al-Khattwaab akadhihirishwa kwangu – alikuwa amevaa kanzu refu ilikuwa ikiburuta.” Wakasema: ”Unaifasirije hiyo, ee Mtume wa Allaah?” Akasema: ”Dini.”[1]

21 – Nuuh bin Habiyb ametukhabarisha: ´Abdur-Razzaaq ametuhadithia: Ma´mar ametukhabarisha, kutoka kwa az-Zuhriy, kutoka kwa Saalim, kutoka kwa baba yake, ambaye amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Wakati nilipokuwa nimelala niliota kuwa naletewa kikombe nikanywa humo mpaka nikaona kinywaji kinatoka nje. Kisha nikampa nilichobaki ´Umar.” Wakasema: ”Unaifasirije hiyo, ee Mtume wa Allaah?” Akasema: ”Dini.”[2]

22 – ´Amr bin ´Uthmaan amenikhabarisha: Baqiyyah ametuhadithia: az-Zubaydiy amenihadithia: az-Zuhriy amenikhabarisha, kutoka kwa Hamzah bin ´Abdillaah bin ´Umar, kutoka kwa Ibn ´Umar, ambaye amesimulia kuwa amemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema:

”Wakati nilipokuwa nimelala niliota napewa kikombe cha maziwa. Nikanywa humo mpaka nikaona kinywaji kinatiririka kwenye kucha zangu. Kisha nikampa nilichobaki ´Umar.” Wakasema: ”Unaifasirije hiyo?” Akasema: ”Dini.”

[1] al-Bukhaariy (23) na Muslim (2390).

[2] al-Bukhaariy (3681) na Muslim (2391).

  • Muhusika: Imaam Ahmad bin Shu´ayb an-Nasaa’iy (afk. 303)
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fadhwaa-il-us-Swahaabah, uk. 40-41
  • Imechapishwa: 03/09/2026