Bora ni mtu kufunga siku sita hizi kwa kufuatanisha ingawa inafaa kuziachanisha muda wa kuwa ni ndani ya mwezi. Kuzifunga mara tu baada ya ´Iyd-ul-Fitwr kumalizika kuna sifa za kipekee kuliko kuzifunga kwa kuachanisha. Hilo ni kwa njia nyingi:
1 – Kufanya hivo kuna kuharakia kufanya mambo ya kheri.
2 – Mtu kuziharakisha ni alama ya shauku yake ya kufunga na kuonyesha kuwa haikumchosha.
3 – Asije kuzukiwa na kikwazo cha kuifunga endapo ataichelewesha.
4 – Kufunga siku sita baada ya Ramadhaan ni kama kuswali Raatibah baada ya swalah ya faradhi, jambo ambalo linakuwa baada yake. Allaah ndiye mjuzi zaidi.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Mukhtaswar Ahaadiyth-is-Swiyaam, uk. 84-85
- Imechapishwa: 08/03/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)