Swali: Ni ipi hukumu ya kumpa zakaah mtu aende kuhiji?
Jibu: Ni vizuri. Kumsaidia mtu kwenda kuhiji ni jambo zuri. Inafaa kumpa zakaah ili mtu aende kuhiji. Kwa sababu hajj ni katika jihaad katika njia ya Allaah. Miongoni mwa aina za watu wanaopewa zakaah ni pamoja na katika njia ya Allaah na hajj ni katika njia ya Allaah na ni katika jihaad. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema alipoulizwa kama inafaa kwa mwanamke kwenda kupigana jihaad ambapo akajibu:
“Ndio. Yuko na jihaad isiyokuwa na mapambano; Hajj na ´Umrah.”
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/eg–14041434.mp3
- Imechapishwa: 28/04/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)