“Yule ni Mtume na yule ni Swahabah”

Swali: Baadhi ya watu na wanafunzi wanaposhauriwa kufanya kama alivofanya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) au Swahabah anasema “Yule ni Mtume” na “Yule ni Swahabah”. Ni ipi nasaha yako kwao?

Jibu: Ndio, ni kweli. Yule ni Mtume na yule ni Swahabah, lakini sisi tumeamrishwa kumuigiliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na Maswahabah. Allaah (Ta´ala) amesema:

لَّقَدْ كَانَ لَكُمْ فِي رَسُولِ اللَّـهِ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ

”Kwa hakika mna kigezo kizuri kwa Mtume Allaah.” (33:21)

وَالسَّابِقُونَ الْأَوَّلُونَ مِنَ الْمُهَاجِرِينَ وَالْأَنصَارِ وَالَّذِينَ اتَّبَعُوهُم بِإِحْسَانٍ رَّضِيَ اللَّـهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا عَنْهُ الْعَظِيمُ

“Wale waliotangulia mwanzoni ambao ni Muhaajiruun na Answaar na wale waliowafuata kwa wema, Allaah ameridhika nao nao wameridhika Naye.” (09:100)

Sisi tumeamrishwa kumuiga Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na Maswahabah zake.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/blug–1430-7-27.mp3
  • Imechapishwa: 19/04/2015