Swali: Je, kuna ubaya kusema:
“Himdi zote njema anastahiki Allaah ambaye hakuna mwingine anayesifiwa kwa yanayochukiza isipokuwa Yeye tu?”
Jibu: Sitambui kuwa ina ubaya. Mtu anaweza kufikwa na jambo lenye kumchukiza, licha ya hivo akamuhimidi Allaah. Akifikwa na maradhi au msiba mwingine akamsifu na kusema:
الحمد لله على كل حال
“Himdi zote njema anastahiki Allaah kwa kila hali.”
إنا لله وإنا إليه راجعون
“Hakika sisi ni wa Allaah na Kwake ndiko tutarejea.”
Allaah (´Azza wa Jall) anasifiwa kwa kila hali, kwa sababu hahukumu hukumu isipokuwa ndani yake kuna kheri na manufaa.
Swali: Kwa hiyo maana yake ni sahihi?
Jibu: Ndio, maana yake ni sahihi.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23145/حكم-قول-الذي-لا-يحمد-على-مكروه-سواه
- Imechapishwa: 11/11/2023
Swali: Je, kuna ubaya kusema:
“Himdi zote njema anastahiki Allaah ambaye hakuna mwingine anayesifiwa kwa yanayochukiza isipokuwa Yeye tu?”
Jibu: Sitambui kuwa ina ubaya. Mtu anaweza kufikwa na jambo lenye kumchukiza, licha ya hivo akamuhimidi Allaah. Akifikwa na maradhi au msiba mwingine akamsifu na kusema:
الحمد لله على كل حال
“Himdi zote njema anastahiki Allaah kwa kila hali.”
إنا لله وإنا إليه راجعون
“Hakika sisi ni wa Allaah na Kwake ndiko tutarejea.”
Allaah (´Azza wa Jall) anasifiwa kwa kila hali, kwa sababu hahukumu hukumu isipokuwa ndani yake kuna kheri na manufaa.
Swali: Kwa hiyo maana yake ni sahihi?
Jibu: Ndio, maana yake ni sahihi.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23145/حكم-قول-الذي-لا-يحمد-على-مكروه-سواه
Imechapishwa: 11/11/2023
https://firqatunnajia.com/yeye-pekee-ndiye-anayesifiwa-kwa-kila-hali/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)