Swali: Kuna sharti zipi zinazotakiwa kutimia katika kichinjwa cha Hadiy na Udhhiyah?
Jibu: Ni lazima awe amesalimika na kasoro, kama alivosema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
”[Wanyama] wanne hawasihi katika wanyama wa Udhhiyah: Mwenye chongo linaloonekana wazi chongo lake, mwenye ugonjwa ambaye ugonjwa wake unaonekana wazi, kiguru ambaye uguru wake unaonekana wazi na mnyonge asiye na mifupa imara.”[1]
Amekataza pia kumchinja Udhhiyah mnyama aliyekatika pembe na sikio. Ni yule mnyama ambaye sehemu yake kubwa ya pembe au sikio imekatika. Ni lazima kuchunga kusalimika kwake na kasoro; ni mamoja ni mnyama wa Hadiy au Udhhiyah.
[1] Abu Dawuud (2785), at-Tirmidhiy (1530), an-Nasaa´iy (7/214) na Ibn Maajah (3144).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/18208/الشروط-الواجب-توافرها-في-الاضحية-والهدي
- Imechapishwa: 11/06/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)