Vipi kuwaunga ndugu walio mbali na wewe?

Swali: Ni yepi makusudio ya kuunga kizazi katika Hadiyth mbalimbali?

Jibu: Kuunga kizazi maana yake ni wale ndugu na jamaa. Ndugu wote ni kizazi chako. Walio karibu zaidi ni baba, mama, watoto na wajukuu.

Swali: Vipi ikiwa mtu anataka kuunga kizazi chake lakini wapo katika nchi nyingine?

Jibu: Anapaswa kuwaunga hata kama wako nchi nyingine. Awaunge kwa kuwaandikia, kuwatumia zawadi na kuwasaidia.

Swali: Kwa hivyo inatosha kuwatumia?

Jibu: Posta zipo.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22281/ما-المراد-بصلة-الرحم-في-الاحاديث
  • Imechapishwa: 27/01/2023