Swali: Kuna bwana mmoja yeye na mke wake wana kafara ya kiapo. Je, azikusanye na kuzitoa kwa pamoja?
Jibu: Kiapo kimoja anatakiwa kuwalisha chakula masikini kumi.
Swali: Ampe mmoja au kumi?
Jibu: Awape masikini kumi. Awatafute hata kama watakuwa magharibi au mashariki mwa ulimwengu.
Swali: Awakusanye?
Jibu: Si lazima kuwakusanya. Anaweza kumlisha mmojammoja. Mmoja anaweza kumpa leo, mwingine akampa mapema, mwingine ´Aqabah, mwingine ar-Riyaadh, mwingine nje ya nchi na mwingine Howtat.
Swali: Ina maana kwamba kafara ya kiapo kimoja inatosha kwa mfano juu ya viapo viwili au viapo vitatu?
Jibu: Inatosha ikiwa ni juu ya kitu kimoja hata kama viapo aliapa mara vingi.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22970/حكم-جمع-عدة-كفارات-يمين-وكيفية-اخراجها
- Imechapishwa: 26/09/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)