Swali: Ni ipi hukumu ya kuswali na viatu?
Jibu: Hapana vibaya. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiswali na viatu.
Swali: Je, ni kwenda kinyume na mayahudi?
Jibu: Ndio, amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Swalini na viatu vyenu. Jitofautisheni nao.”
Lakini watu wengi hawajali misikiti iliyotandikwa mazulia na wanayachafua. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliswali na viatu na aliswali bila ya viatu. Hilo khaswa pale ambapo mtu anakhofia kuchafua msikiti… kwa sababu wengi ni wajinga na hawajali.
Swali: Kwa hivyo haina neno mtu akaswali na viatu na akaswali peku?
Jibu: Hapana neno. Ikiwa msikiti umetandikwa mazulia asiyachafue na kuwafanya watu kuikimbia misikiti.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22957/ما-حكم-الصلاة-بالنعال
- Imechapishwa: 25/09/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)