Swali: Kuna wanaosema kuwa haina neno kuwa na rafiki ambaye ni Shiy´iy au myahudi kwa kutumia hoja ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimtembelea kijana wa kiyahudi.
Jibu: Alimtembelea kwa ajili ya kumlingania katika dini ya Allaah na akamwambia:
“Shuhudia ya kwamba hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah.”
Akamwangalia kwanza baba yake ilihali anataka kukata roho. Baba yake kijana akamwambia:
“Msikilize Abul-Qaasim.”
Ndipo yule kijana akasema:
“Nashuhudia ya kwamba hakuna mungu wa haki isipokuwa Allaah.”
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akawaambia Maswahabah zake:
“Mshughulikieni ndugu yenu.”
Kwa kuwa ameingia katika Uislamu. Mtu kama huyu anasimamiwa na waislamu katika kumuosha, kumvika sanda, kumswalia na kumzika. Alimtembelea kwa ajili ya kumlingania katika Uislamu.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Tafsiyr-ish-Shaykh Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (26) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tafsir%20ayat-03-08-1435-01.mp3
- Imechapishwa: 21/06/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)